SUD-KIVU: Msemaji wa jeshi wa opération sokola ya 2 apata uhamisho
Écrit par FiziMedia sur janvier 22, 2022

Mabadilishano kati ya msemaji wa sekta ya utendakazi sukola ya 2 kusini mwa kivu, Meja Dieudonné Kasereka, na msemaji mpya, luteni ELONGO KYENDWA MARC yamefanyika Siku ya Tano hii, Januari 21, 2022 kwenye uongozi wa jeshi jijini Uvira.
Miaka mitatu,meja Dieudonné Kasereka ametumika kama msemaji wa kijeshi, kwenye opération sokola ya 2 kusini mwa Jimbo ya kusini.
Meja Dieudonné, alihamishiwa kwenye ikulu la Jeshi la maji huko Kinshasa kwa uamuzi wa mamlaka ya kijeshi.
Msemaji huyo mpya anatoka GEMENA ambako alishikilia wadhifa huo.
Meja Dieudonné Kasereka, anawashukuru wanajeshi na mamlaka za kiraia za sehemu ya kusini ya Kivu ya Kusini, kwa ushirikiano wao, ambao ulimwezesha kufanikisha kazi yake.
Anavishukuru vyombo vya habari vya ndani, kitaifa na kimataifa kwa msaada wao.
«Ninaomba kila mtu aendelee
fanya kazi na mbadala wangu,
kwa wanajeshi, uhamisho ni kitu cha kawaida»,amemaliziya kusema ,meja Dieudonné Kasereka.
Fizimedia.com