UBWARI-FIZI : mama mmoja ajulikanaye kwa jina la EKYOCI maharufu MACHOKOSHI ameweza kushikiliwa pamoja na mume wake kijijini KIBANGA na askari jeshi wa taïfa
Écrit par FiziMedia sur février 17, 2019
BUMA-KIBANGA
Mchana wa leo 16/02/2019 mama mmoja ajulikanaye kwa jina la EKYOCI maharufu MACHOKOSHI ameweza kushikiliwa pamoja na mume wake kijijini KIBANGA na askari jeshi wa taïfa kwa tuhuma za kufanyiya wezi wanao pora kwa kutumiya bunduki dawa.
Hayo yametokeya pale ambapo askari waliweza kuwakamata wezi hao pale kijijini BUMA(kijiji kipatikanacho ndani ya nusu kisanga cha ubwari umbali wa kilomita zisizo punguwa sita,6km na kijiji cha KARAMBA) ,Na hapo baada ya kukamatwa ndipo wezi hao walieleza ya kwamba kama wao wana pata nguvu ya kupora ni sababu ya dawa anayo wapa mama huyo, na hiyo ndiyo chanzo cha kushikiliwa kwa mama huyo.
Duru za Habari zinaeleza ya kwamba ,ni baada ya wezi kumkorofisha mama huyo ndipo alipo punguza nguvu za dawa,na matokeo ni kukamatwa,ali heleza jambazi mmoja. Mengi kesho.
fizimedia.com fizimediatv@gmail.com